Mahasimu wakuu wa soka nchini Tanzania, Simba SC na Yanga SC, wanatarajiwa kuanza kuchochea moto wa msimu mpya wa Ligi Kuu NBC 2025/2026 kwa staili ya kipekee.
Kwa mujibu wa ratiba rasmi iliyotolewa na Bodi ya Ligi (TPLB), timu hizi zitakutana kwa mara ya kwanza katika fainali ya Ngao ya Jamii itakayofanyika Septemba 16, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, kuanzia saa 11:00 jioni, na mechi hiyo itarushwa mubashara kupitia AzamSports1HD.
Mechi hii ya Ngao ya Jamii ndiyo itakayopiga jalambo la msimu mpya, huku mashabiki wa kandanda wakisubiri kwa hamu kuona nani ataibuka kidedea kati ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu na washindi wa Kombe la FA.
Ratiba ya Dabi ya Kariakoo 2025/2026 | Tarehe za Mechi za Simba Vs Yanga
Kwa mashabiki wa Dabi ya Kariakoo, hadi sassa msimu huu unatoa mechi tatu kubwa za kukata na shoka kati ya vigogo hawa.
Ikumbukwe pia vigogo hawa wanaweza kukutana kwenye michuano mengine ambayo bado ratiba yake haijatangazwa ikiwemo kombe la FA la Tanzania.
- Ngao ya Jamii: Septemba 16, 2025 – Benjamin Mkapa, Dar es Salaam
- Ligi Kuu NBC (Duru ya Kwanza): Desemba 13, 2025 – Benjamin Mkapa, Yanga wakiwa wenyeji
- Ligi Kuu NBC (Duru ya Pili): Aprili 4, 2026 – Benjamin Mkapa, Simba wakiwa wenyeji
Hii ndiyo ratiba inayotarajiwa kuandika historia mpya ya Dabi ya Kariakoo 2025/2026, huku kila mechi ikitarajiwa kuwa na ushindani mkubwa na mvuto wa aina yake kutoka kwa mashabiki ndani na nje ya Tanzania.