Droo ya Klabu Bingwa Afrika 2025/2026 CAF Champions League

WhatsApp Group Join Now
Telegram Group Join Now

Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika (CAF Champions League) msimu wa 2025/2026 yamezinduliwa rasmi kwa kufanyika kwa droo ya Raundi ya Awali, ikifungua ukurasa wa kwanza wa safari ya kusaka taji kubwa zaidi la soka la vilabu barani Afrika.

Droo hiyo imeweka wazi wapinzani wa timu 60 zilizofuzu hatua ya awali, huku mechi zikitarajiwa kuchezwa kwa mikondo miwili kuanzia tarehe 19–21 Septemba na marudiano tarehe 26–28 Septemba 2025.

Timu zitakazoshinda katika hatua hii zitapiga hatua kwenda Raundi ya Pili ya Mchujo itakayofanyika katikati ya mwezi Oktoba, hatua ambayo itakaribisha vigogo wawili wa soka barani Al Ahly ya Misri na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ambao wamepatiwa mapumziko ya hatua ya kwanza kutokana na nafasi zao za juu kwenye viwango vya CAF.

Wapeperusha Bendera ya Tanzania na Ratiba Zao

Katika droo hii, Tanzania imewakilishwa na miamba miwili ya soka ambayo ni timu ya wananchi Yanga SC na wekundu wa msimbazi Simba SC, ambao wote wamepangwa kuanzia Raundi ya Awali kwa mechi za kwanza ugenini.

  • Yanga SC watakabiliana na Wiliete Benguela ya Angola.
  • Simba SC wao watavaana na Gaborone United ya Botswana.
SOMA HII  Refa Aliyekataa Goli la Aziz Yanga Kusimamia VAR Taifa Stars Vs Morocco

Kwa upande wa Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC imepangwa kuanza dhidi ya Al Merriekh ya Sudan, huku Singida Black Stars wakikabiliana na Rayon Sports ya Rwanda inayoongozwa na kocha wa zamani wa Simba, Robertinho Oliveira.

Msimu uliopita, Yanga iliishia hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, huku Azam FC ikijikuta ikitolewa mapema kwenye hatua ya awali ya Kombe la Shirikisho. Simba, licha ya historia yao nzuri katika michuano ya CAF, walimaliza kama washindi wa pili kwenye Kombe la Shirikisho baada ya kuchechezea kichapo kutoka kwa RS Berkane.

Kwa Singida Black Stars, hii ni mara yao ya kwanza kushiriki mashindano ya kimataifa, wakiendeleza nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Coastal Union. Wamekuwa wakitarajiwa kufanya vyema kutokana na uwekezaji mkubwa walioufanya, pamoja na uongozi wa Kocha Miguel Gamondi ambaye aliifikisha Yanga hatua ya makundi msimu uliopita.

SOMA HII  Yanga SC Kucheza Dhidi ya Bandari FC Siku ya Wiki ya Mwananchi 2025

Droo ya Klabu Bingwa Afrika 2025/2026: Timu na Ratiba Ya Round ya Awali

Orodha ya Mechi Zote za Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika 2025/2026

  • Ethiopian Insurance (Ethiopia) vs Mlandege (Zanzibar)
  • APR FC (Rwanda) vs Pyramids FC (Egypt)
  • Mogadishu City (Somalia) vs Kenya Police (Kenya)
  • Jamus FC (South Sudan) vs Al Hilal (Sudan)
  • Rahimo FC (Burkina Faso) vs Mangasport (Gabon)
  • AS FAN (Niger) vs Espérance (Tunisia)
  • Dadje FC (Benin) vs Libya 1 (Libya)
  • ASCK (Togo) vs RS Berkane (Morocco)
  • East End Lions (Sierra Leone) vs US Monastir (Tunisia)
  • Goldstars (Ghana) vs JS Kabylie (Algeria)
  • Fundacion Bata (Equatorial Guinea) vs Nouadhibou (Mauritania)
  • AS Tempete (CAR) vs Stade Malien (Mali)
  • Libya 2 (Libya) vs Horoya AC (Guinea)
  • DR Congo 2 (DR Congo) vs Al Merriekh (Sudan)
  • Colombe Sportive (Cameroon) vs ASC Jaraaf (Senegal)
  • FC Fassell (Liberia) vs MC Alger (Algeria)
  • Remo Stars (Nigeria) vs Zilimadjou (Comoros)
  • Simba Bhora (Zimbabwe) vs Nsingizini Hotspurs (Eswatini)
  • Gaborone United (Botswana) vs Simba SC (Tanzania)
  • Elgeco Plus (Madagascar) vs Silver Strikers (Malawi)
  • Wiliete Benguela (Angola) vs Yanga SC (Tanzania)
  • Cote d’Or (Seychelles) vs Stade d’Abidjan (Ivory Coast)
  • Cercle Joachim (Mauritius) vs Petro Atletico (Angola)
  • AC Leopards (Congo) vs Black Bulls (Mozambique)
  • DR Congo 1 (DR Congo) vs Rivers United (Nigeria)
  • African Stars (Namibia) vs Vipers SC (Uganda)
  • Power Dynamos (Zambia) vs ASEC Mimosas (Ivory Coast)
  • Lioli FC (Lesotho) vs Orlando Pirates (South Africa)
SOMA HII  Droo ya Kombe la Shirikisho CAF 2025/2026 | CAF Confederation Cup

Hot this week

Nafasi za Kazi Jeshi la Magereza 2025

Jeshi la Magereza limetangaza nafasi mpya za ajira kwa...

Namna Ya Kuangalia Taarifa Za Usajili NIDA | Hatua kwa hatua

Namna Ya Kuangalia Taarifa Za Usajili NIDA, Kuangalia taarifa...

Mfumo wa Maombi ya Ajira kwa Walimu Mtandaoni (OTEAS)

Mwongozo wa Mfumo wa Maombi ya Ajira kwa Walimu...

Orodha ya Vifurushi vya Azam TV na Bei zake – Chagua Kifurushi Kinachokufaa

Azam TV imekuwa sehemu muhimu ya burudani ndani ya...

Sample/Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi Jeshi la Magereza

Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi Jeshi la...

Wasifu CV ya Neo Maema Kiungo Mpya wa Simba 2025/2026

Klabu ya Simba SC imethibitisha kukamilisha usajili wa kiungo...

Wasifu CV Ya Mohamed Doumbia Kiungo Mpya wa Yanga 2025/2026

Mu Ivory Coast, Mohamed Doumbia (26) ametambulishwa na timu...

Ratiba ya Klabu Bingwa Afrika 2025/2026 Hatua ya Awali

Droo ya mashindano ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF)...

Timu 12 Zitakazoshiriki Mashindano ya CECAFA Kagame Cup 2025

Timu 12 Zitakazoshiriki Mashindano ya CECAFA Kagame Cup 2025 Timu...

Orodha ya Wafungaji Bora CHAN 2025

Orodha ya Wafungaji Bora CHAN 2025, Michuano ya CHAN...

Kikosi cha Taifa Stars vs Morocco Leo 22 August 2025 CHAN

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ itacheza mchezo...

Wasifu CV Ya Rushine De Reuck Beki Mpya wa Simba 2025/2026

Klabu ya Simba imemtambulisha rasmi beki wa kati, Rushine...

Related Articles

Popular Categories

Njia Rahisi ya Kuangalia Namba ya NIDA Kwa SMS

Njia Rahisi ya Kuangalia Namba ya NIDA Kwa SMS, Kupata namba ya NIDA kwa njia ya SMS ni rahisi na haraka. Njia hii ni...

Jinsi ya Kupata Mtoto wa Kiume

Jinsi ya Kupata Mtoto wa Kiume, Ni shauku ya kila mzazi kupata Watoto wa Jinsia tofauti katika uzao wao ingawaje Wengi hupata watoto wa...

Jinsi ya Kukopa Muda wa Maongezi Halotel | Menu ya kukopa Salio Halotel

Jinsi ya Kukopa Muda wa Maongezi Halotel, Je Unatumia mtandao wa simu wa halotel na umekwama na hujui hatua ,sifa na vigezo za kupata...