Wasifu CV Ya Mohamed Doumbia Kiungo Mpya wa Yanga 2025/2026

WhatsApp Group Join Now
Telegram Group Join Now

Mu Ivory Coast, Mohamed Doumbia (26) ametambulishwa na timu ya Yanga sc kuwa sehemu ya safu yao ya kati. Usajili huu unaongeza nguvu mpya katika kikosi cha mabingwa hao wa Tanzania Bara, huku ukiongeza ushindani mkubwa ndani ya timu.

Wasifu CV Ya Mohamed Doumbia Kiungo Mpya wa Yanga 2025/2026

CV Ya Mohamed Doumbia Kiungo Mpya wa Yanga 2025/2026

Wasifu wa Mohamed Doumbia

Mohamed Doumbia alizaliwa tarehe 25 Desemba, 1998 katika jiji la Abidjan, Ivory Coast. Kiungo huyu mwenye urefu wa 1.74 mita hutumia mguu wa kulia kama mguu wake wa msingi uwanjani. Ana uraia wa Ivory Coast na anacheza katika nafasi ya Kiungo wa Kati.

SOMA HII  Wasifu CV ya Romain Folz Kocha Mpya wa Yanga 2025/2026

Kwa takribani muongo mmoja, Doumbia ameonesha uwezo mkubwa katika safu ya kiungo, akicheza katika ligi mbalimbali barani Ulaya na Afrika, na sasa anatarajiwa kuleta uzoefu huo mkubwa ndani ya kikosi cha Yanga SC msimu ujao.

Historia ya Uhamisho wa Mohamed Doumbia

CV ya Mohamed Doumbia kiungo mpya wa Yanga 2025/2026 inaonesha mchezaji mwenye uzoefu mpana katika soka la kimataifa, akiwa amepitia vilabu kadhaa vya ushindani:

Msimu Tarehe ya Uhamisho Aliyetoka Aliyejiunga Thamani ya Soko Ada ya Uhamisho
2024/2025 17 Machi 2025 SC Majestic Bila Klabu €350k Bure
2024/2025 28 Januari 2025 Bila Klabu SC Majestic €350k Bure
2024/2025 01 Julai 2024 Slovan Liberec Bila Klabu €400k Bure
2021/2022 17 Februari 2022 Dukla Prague Slovan Liberec €150k Uhamisho Huru
2017/2018 01 Januari 2018 Ekenäs IF Dukla Prague €50k €50k
2016/2017 01 Januari 2017 Haijulikani Ekenäs IF Haijatajwa Uhamisho Huru
SOMA HII  Refa Aliyekataa Goli la Aziz Yanga Kusimamia VAR Taifa Stars Vs Morocco

Kwa mujibu wa historia yake, Doumbia amewahi kuitumikia vilabu vya SC Majestic (Burkina Faso), Slovan Liberec na Dukla Prague (vyote vya Jamhuri ya Czech), pamoja na Ekenäs IF ya Finland. Safari yake ya soka inaonesha mchezaji mwenye uthabiti wa kiufundi, aliyezoea kushindana katika mazingira tofauti ya ligi mbalimbali.

Safari Yake ya Kitaaluma

  • 2017-2018: Doumbia alianza safari yake ya kimataifa barani Ulaya alipokuwa Ekenäs IF nchini Finland.
  • 2018-2022: Baada ya Finland, aliingia katika soka la Jamhuri ya Czech akijiunga na Dukla Prague ambapo alidumu kwa takribani miaka minne kabla ya kuhamia Slovan Liberec.
  • 2024-2025: Alirejea barani Afrika na kujiunga na SC Majestic ya Burkina Faso kabla ya kuachana na klabu hiyo Machi 2025.
  • 2025: Hatimaye, amejiunga rasmi na Yanga SC kama mchezaji huru.
SOMA HII  Times FM Kutangaza Mubashara Kagame Cup 2025, Kuanzia Tarehe 2 Septemba 

Sehemu ya Usajili Mpya Yanga SC 2025/2026

Mohamed Doumbia anakuwa mchezaji wa nane mpya kusajiliwa na Yanga SC kwa msimu wa 2025/2026, na mchezaji wa tano wa kigeni katika kikosi hicho. Wengine waliotangulia ni:

  1. Lassine Kouma – Kiungo kutoka Stade Malien, Mali
  2. Balla Mousa Conte – Kiungo kutoka CS Sfaxien, Tunisia
  3. Andy Bobwa Boyeli (24) – Mshambuliaji kutoka Sekhukhune United FC, Afrika Kusini
  4. Ange Celestin Ecua – Mshambuliaji kutoka Zoman FC, Ivory Coast

Kwa upande wa wazawa, Yanga pia imesajili wachezaji wafuatao:

  1. Abdulnasir Mohamed Abdallah – Kiungo kutoka Mlandege, Zanzibar
  2. Nizar Abubakar Othman ‘Ninju’ – Kiungo kutoka JKU, Zanzibar
  3. Offen Francis Chikola – Winga kutoka Tabora United

Hot this week

Nafasi za Kazi Jeshi la Magereza 2025

Jeshi la Magereza limetangaza nafasi mpya za ajira kwa...

Namna Ya Kuangalia Taarifa Za Usajili NIDA | Hatua kwa hatua

Namna Ya Kuangalia Taarifa Za Usajili NIDA, Kuangalia taarifa...

Mfumo wa Maombi ya Ajira kwa Walimu Mtandaoni (OTEAS)

Mwongozo wa Mfumo wa Maombi ya Ajira kwa Walimu...

Orodha ya Vifurushi vya Azam TV na Bei zake – Chagua Kifurushi Kinachokufaa

Azam TV imekuwa sehemu muhimu ya burudani ndani ya...

Sample/Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi Jeshi la Magereza

Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi Jeshi la...

Wasifu CV ya Neo Maema Kiungo Mpya wa Simba 2025/2026

Klabu ya Simba SC imethibitisha kukamilisha usajili wa kiungo...

Ratiba ya Klabu Bingwa Afrika 2025/2026 Hatua ya Awali

Droo ya mashindano ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF)...

Timu 12 Zitakazoshiriki Mashindano ya CECAFA Kagame Cup 2025

Timu 12 Zitakazoshiriki Mashindano ya CECAFA Kagame Cup 2025 Timu...

Orodha ya Wafungaji Bora CHAN 2025

Orodha ya Wafungaji Bora CHAN 2025, Michuano ya CHAN...

Kikosi cha Taifa Stars vs Morocco Leo 22 August 2025 CHAN

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ itacheza mchezo...

Wasifu CV Ya Rushine De Reuck Beki Mpya wa Simba 2025/2026

Klabu ya Simba imemtambulisha rasmi beki wa kati, Rushine...

Matokeo ya Taifa Stars vs Morocco Leo 22/08/2025 CHAN

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars,...

Related Articles

Popular Categories

Njia Rahisi ya Kuangalia Namba ya NIDA Kwa SMS

Njia Rahisi ya Kuangalia Namba ya NIDA Kwa SMS, Kupata namba ya NIDA kwa njia ya SMS ni rahisi na haraka. Njia hii ni...

Jinsi ya Kupata Mtoto wa Kiume

Jinsi ya Kupata Mtoto wa Kiume, Ni shauku ya kila mzazi kupata Watoto wa Jinsia tofauti katika uzao wao ingawaje Wengi hupata watoto wa...

Jinsi ya Kukopa Muda wa Maongezi Halotel | Menu ya kukopa Salio Halotel

Jinsi ya Kukopa Muda wa Maongezi Halotel, Je Unatumia mtandao wa simu wa halotel na umekwama na hujui hatua ,sifa na vigezo za kupata...